mo dadyTV

KARIBU KUTANGAZA NASI 0652231836

kARIBU KUTANGAZA NASI 0652231836

LightBlog
KARIBU KUTANGAZA NASI 0652231836

Karibu kutangaza nasi mawasiliano 0652231836

Jumatatu, 10 Julai 2017

Waziri wa zamani wa Nishati na Madini na Mbunge wa Sengerema CCM, William Ngeleja ametangaza kurejesha pesa za ESCROW, kiasi cha Tsh. mil. 40.4 alizopokea kutoka kwa James Rugemalira anayetuhumiwa katika sakata la ESCROW tarehe 12 Februari 2014. Ngeleja amewaambia wanahabari leo kuwa,tayari amerudisha TRA TSh 40.4milioni alizokuwa amepewa na mfanyabiashara James Rugemalila.

Jumatatu, 26 Juni 2017

Producer bora toka Arusha aliewai kuproduce hit song nying ikiwemo nishuke wapi ya real voice inasemekana kudaiwa kuachana na mpenzi wake aliekuwa akijulikana kwa jina la Johari na sasa hupo katika wimbi la mapenzi mazito na kigori mmoja huko arusha ambaye atukuweza kumjua jina Wawili hao wamekuwa wakioneka sehemu mbalimbali za bata...
Mo fravour
Blog yetu inaendelea kunafanya juhudi za kumtafuta Johari ili atusibitishie ameachana na Mo Flavour au la



Ijumaa, 23 Juni 2017

MKUU wa Wilaya ya Shinyanga, Josephine Matiro amelazimika kula chakula na kunywa maji yaliyotoka kwenye mradi wa maji wa kisima kirefu uliokataliwa na wananchi kwa hofu kuwa wakinywa maji hayo watakufa na wakipikia chakula kitabadilika rangi ya njano.
Mkuu huyo akiwa kwenye mkutano wa hadhara katika kijiji hicho juzi alitaka kusikiliza kero za wananchi na kufahamu kwanini wanaendelea kutumia maji ambayo siyo safi na salama ikiwa mradi upo tangu mwaka 2014 hawajawahi kuyatumia.
Matiro aliyekuwa ameambatana na Kamati ya Ulinzi na Usalama na viongozi wengine na baada ya kusikiliza hoja hiyo walilazimika kuyaonja na kupika chakula kwa haraka na kubainika hayana chumvi wala chakula kilichopikwa kutokuwa cha njano ndipo ilipobainika kuwa walidanganywa kwa sababu za kisiasa.

Jumatatu, 19 Juni 2017

WATANZANIA wametakiwa kutoa taarifa wanabaini uwepo wa mchele usioeleweka, baada ya kuibuka kwa taarifa ya mchele bandia wa plastiki kukamatwa Nigeria.
Msemaji wa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA), Gaudencia Simwanza alisema hayo jana .
Alisema wao sasa wana mifumo mizuri ya kudhibiti uingizwaji wa bidhaa zisizofaa na mpaka sasa mfumo huo haujabaini mchele wa aina hiyo nchini.
"Tunadhibiti na tuko makini kufuatilia wafanyabiashara wanaoingiza vitu haramu na kama huo mchele ungekuwa umeingia, tungeshajua," alisema.
Mwandishi wa habari hii alipomwuliza ikitokea umeingizwa kimagendo nchini, Watamzania watautambua vipi, Gaudencia aliwataka kutoa ushirikiano kwa kutoa taarifa watakapoona mchele wasiouelewa.
Mchele huo bandia ulikamatwa na Mamlaka ya Mji wa Lagos, Nigeria wiki hii, ambapo walikamata magunia 102.
Taarifa kutoka nchini humo, zilieleza kuwa uliingizwa nchini humo na wafanyabiashara haramu na unafanana na mchele wa kawaida, hivyo ni ngumu kuutofautisha na mchele wa kawaida.
Kutokana na kusambaa kwa kasi kwa mchele huo, huwezi kuutambua kwa haraka hadi pale unapopikwa ndipo unaweza kuona ni mchele wa plastiki. Hata hivyo baadhi ya wataalamu walisema kabla ya kuupika mchele huo ukilowekwa kwenye chombo chenye maji unaelea tofauti na halisi ambao huzama.
Hospitali ya Muhimbili imemkamata kijana aliyejifanya Daktari na kuanza kuhudumia watu idara ya benki ya damu hospitalini hapo.Msemaji wa Hospitali yaTaifa Muhimbili Aminiel Eligaesha, amesema kuwa huo ni mwendelezo wa kuwakamata vishoka ndani ya Hospitali hiyo.Picha ya Gazeti la #Mwananchi
 

Jumatano, 14 Juni 2017

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mh. Ally Hapi ameendelea na juhudi za utatuzi wa migogoro ya ardhi ambayo inahusisha wananchi wenye mashamba katika maeneo ya Kinondo, Dovya na Mbopo.
Juhudi hizo zimedhihirika Leo katika kikao kilichofanyika kwenye ukumbi wa Manispaa kilichohusisha wananchi pamoja na wataalam wa Mipangomiji kwa kuwaahidi wananchi hao kumaliza mgogoro hiyo ili waweze kuishi kwa amani.
Hapi amesema dira ya Wilaya ya Kinondoni ni kuhakikisha viwanja vyote vinapimwa ili kuweka mipango mizuri ya matumizi ya Ardhi itakayozuia uvamizi wa mashamba pamoja na maeneo ya wazi.
Aidha amewataka wale wote wanaomiliki maeneo hayo kuyaendeleza baada ya kufanyiwa upimaji ili kuepusha migogoro ya mipaka inayoweza kutokea.
Migogoro mingine inayoendelea kutatuliwa ni pamoja na TBA Mabwepande na Nyakasangwe ambayo kwa sasa maeneo hayo yamefikia hatua ya upimaji viwanja.
Mkuu wa wilaya ya kinondoni Ally Hapi
Rais mstaafu Dk Jakaya Mrisho kikwete amehudhuria mkutano wa kwanza wa Baraza la Wakimbizi Duniani mjini Geneva Uswisi akiwa mmoja wa wenyeviti wa baraza hilo.

Jumamosi, 10 Juni 2017

Producer bora toka arusha anaejulikana kwa jina la mo flavour baada ya mda mrefu kutuficha kuwa hana mahusiano na mwanamke yeyote leo tumepokea taarifa toka kwa papalazi mmoja na usibitisho kuwa mo Flavour ana mahusiano na bint mmoja mwenye asili ya kihind anaeitwa Johari
Johari
Mo flouvar na Johari
Papalazi huyo alituleza kuwa johari na mo flavour wanapendana sana na wanaonekana mara kwa mara wakiwa pamoja
Leo ktk ukumbi wa chek point pale kigogo fresh kulikuwa na kikao cha semina elekezi kwa viongozi wa Uvccm .Dhumuni la semina hiyo elekezi ni kutoa maelekezo kwa viongozi wapya waliochaguliwa nini chama chao kinaitaji pia kujua mipaka ya uongozi wao bila kusahau kujua maadili ya chama chao..

Mgeni rasmi katibu mkoa wa Dar es salaam
Said Yassin
Watoa mada
Mashaka Nyadhi

Frank Mang'ati 
Mwenyekiti Uvccm wilaya ya ilala
alfrd Tukiko

Alhamisi, 8 Juni 2017

Dr Ulimboka alikuwa mwenyeki wa taasisi ya Madaktari nchini Tanzania, Dr ulimboka alitisha mgomo wa madaktali nchi nzima usio na kikomo tar 24 jun 2012 kwa madai ya Serikali imekataa madai yao yote walio wasilisha katika kamati ya majadiliano iliyoundwa na waziri mkuu mstaafu Mizengo pinda.....
Wakati mgomo ukiendelea tar 27 ucku zilipatikana taarifa za kutekwa kwa Dr ulimboka na hakuna mtu alie jua alitekwa na nani na yupo wapi baada ya cku kazaa Dr ulimboka alipatikana katika msituni akiwa amelowa damu kutokana na kipigo kikali
  


Dr ulimboka

inasemekana Dr ulimboka alipata mateso makali kutoka kwa watekahi hao .

MJUE ALIE MTEKA DR ULIMBOKA
Baada ya siku kazaa kupita gazeti la mwanahalisi lilitoa taarifa za alie mteka Dr ulimboka nazo ni hizi hapa chini

Kutoka Mwanahalisi:
Waliomteka dr. Ulimboka hawa hapa
Anaitwa RAMADHANI IGHONDU, a.k.a RAMA ni afisa Usalama wa Taifa(TISS) anayefanyia kazi zake ikulu katika idara ya siasa chini ya Zoka, MwanaHALISI linaeleza. Kachero huyo (RAMA) ndiye aliekuwa akijitambulisha kama ABEID wa ikulu na alikutana na ulimboka tangu mgogoro wa kwanza wamadaktari. Rekodi katika simu ya Ulimboka 0713731610, inaonyesha Rama ndiye alikuwa mtu wa mwisho kufanya naye mawasiliano Saa 5;52 kwa kupitia simu yake (RAMA) 0713760473, muda mchache kabla ya kutekwa kwa ulimboka.
Kabla ya ULIMBOKA kutekwa, RAMA alifanya naye mazungumzo saa12:25 jioni, saa 3:29 usiku, saa 4:52, saa 5:27, saa 5:40 na mwiso ilikuwa saa 5:52 usiku na mwenye namba hiyo ndiye aliyeandaa kukutana na ULimboka usiku naye (ULIMBOKA) amethibitisha bila shaka yeyote kuitambua namba hiyo ya ABEID.
Kabla ya namba hiyo kufanya mawasiliano na Ulimboka saa 12:25 ilifanya mawasiliano na BURUANI NTILONGWA (0712359533) pia kati ya saa 2:08 na 2:24 usiku. Aitha mwandishi (KUBENEA) anasema ripoti yake inaonyesha kila muda ambao RAMA alikuwa akifanya mazungumzo na Ulimboka pia alifanya mawasiliano na MOSHI MARUNGU SHABANI (0761132663 & 0655162663), ABDALLAH KUNJA na NTILONGWA. Siku mbili kabla ya kutekwa ulimboka simu ya RAMA iliingiziwa (airtime) salio la tshs 252,849/- ambalo ni salio kubwa kuingizwa tangu mwanzo mwa mwaka huu ukizingatia tarehe 04 Mei mwaka huu simu ya Rama ilikuwa na Tshs.01. Wengine waliokuwa na mawasiliano ya mara kwa mara na RAMA kabla ya kutekwa Ulimboka ni; Mohamed Hassan 0655524444, Shomari Kondo 0714666304. Optat Jacob Marandu 0716611625 na Mbega Hisbert 0715222778.
Taarifa nyingine kutoka ndani ya Tiss zinasema agent RAMA, tangu tarehe 26 Juni 2012 baada ya kufanikiwa kwa jaribio la kumteka Ulimboka, RAMA aliacha kutumia simu yake hiyo. Na tarehe 01 july amekuwa akituma sms kwa namba nne tofauti kwa zaidi.
Wakati wakimtesa Ulimboka ni RAMA aliyekuwa akisisitiza kuelezwa ni nani hasa katika CHADEMA aliyemtumia. Wazo lililopo Usalama wa Taifa ni kuwa Ulimboka anatumiwa na Mnyika pamoja na Dr. Slaa. Chini ya Zoka, wanatakiwa kuangamizwa hasa wale wanao ikosoa sana serikali.
Nukuu kutoka mwanahalisi.

Kutoka Mwanahalisi:
Waliomteka dr. Ulimboka hawa hapa

Anaitwa RAMADHANI IGHONDU, a.k.a RAMA ni afisa Usalama wa Taifa(TISS) anayefanyia kazi zake ikulu katika idara ya siasa chini ya Zoka, MwanaHALISI linaeleza. Kachero huyo (RAMA) ndiye aliekuwa akijitambulisha kama ABEID wa ikulu na alikutana na ulimboka tangu mgogoro wa kwanza wamadaktari. Rekodi katika simu ya Ulimboka 0713731610, inaonyesha Rama ndiye alikuwa mtu wa mwisho kufanya naye mawasiliano Saa 5;52 kwa kupitia simu yake (RAMA) 0713760473, muda mchache kabla ya kutekwa kwa ulimboka.

Kabla ya ULIMBOKA kutekwa, RAMA alifanya naye mazungumzo saa12:25 jioni, saa 3:29 usiku, saa 4:52, saa 5:27, saa 5:40 na mwiso ilikuwa saa 5:52 usiku na mwenye namba hiyo ndiye aliyeandaa kukutana na ULimboka usiku naye (ULIMBOKA) amethibitisha bila shaka yeyote kuitambua namba hiyo ya ABEID.

Kabla ya namba hiyo kufanya mawasiliano na Ulimboka saa 12:25 ilifanya mawasiliano na BURUANI NTILONGWA (0712359533) pia kati ya saa 2:08 na 2:24 usiku. Aitha mwandishi (KUBENEA) anasema ripoti yake inaonyesha kila muda ambao RAMA alikuwa akifanya mazungumzo na Ulimboka pia alifanya mawasiliano na MOSHI MARUNGU SHABANI (0761132663 & 0655162663), ABDALLAH KUNJA na NTILONGWA. Siku mbili kabla ya kutekwa ulimboka simu ya RAMA iliingiziwa (airtime) salio la tshs 252,849/- ambalo ni salio kubwa kuingizwa tangu mwanzo mwa mwaka huu ukizingatia tarehe 04 Mei mwaka huu simu ya Rama ilikuwa na Tshs.01. Wengine waliokuwa na mawasiliano ya mara kwa mara na RAMA kabla ya kutekwa Ulimboka ni; Mohamed Hassan 0655524444, Shomari Kondo 0714666304. Optat Jacob Marandu 0716611625 na Mbega Hisbert 0715222778.

Taarifa nyingine kutoka ndani ya Tiss zinasema agent RAMA, tangu tarehe 26 Juni 2012 baada ya kufanikiwa kwa jaribio la kumteka Ulimboka, RAMA aliacha kutumia simu yake hiyo. Na tarehe 01 july amekuwa akituma sms kwa namba nne tofauti kwa zaidi.
Wakati wakimtesa Ulimboka ni RAMA aliyekuwa akisisitiza kuelezwa ni nani hasa katika CHADEMA aliyemtumia. Wazo lililopo Usalama wa Taifa ni kuwa Ulimboka anatumiwa na Mnyika pamoja na Dr. Slaa. Chini ya Zoka, wanatakiwa kuangamizwa hasa wale wanao ikosoa sana serikali.

Nukuu kutoka mwanahalisi.
ushuhuda wa Dr Ulimboka
Rais Jakaya Kikwete azungumzia

Jumapili, 28 Mei 2017

Jumamosi, 27 Mei 2017

Rais wa Makampuni *CNBM*  kutoka Beijing CHINA *Bw. Cao Jiang Lin* amekutana na kufanya mazungumzo na Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam *Mhe Paul Makonda,* jiji Dar es salaam.

Katika mazungumzo hayo, *Bw. Lin* amemuhakikisha mkuu wa mkoa *Mhe Makonda* kuwa makampuni mengi yameonyesha nia ya dhati ya kuja kuwekeza *Tanzania* na Dar es salaam ambapo tayari baadhi ya makampuni yameshaanza kuwekeza jijini *Dar es salaam.*

Katika Mazungumzo yao, *Bw. Lin* amemuahidi Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam *Mhe Makonda* kuwapatia *kazi vijana wa Dar es salaam zaidi ya  500* kupitia ofisi ya Mkuu wa Mkoa.

Ikumbukwe makampuni ya *CNBM* yako zaidi ya *500 duniani* na ndiyo makampuni yanayoongoza kwa uzalishaji wa cement na bidhaa zaidi ya *15,000 DUNIANI.*


*Imetolewa na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam.*
*27/05/2017*
Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe amesema chama chake kinamuunga mkono Uhuru Kenyatta ktk Uchaguzi Mkuu mwaka huu.

Amesema kuwa kwa muda mrefu wamekuwa wakimuunga mkono Raila Odinga katika kuchukua nafasi ya kuiongoza Kenya.

Lakini kinyume na matarajio yao, ilipofika zamu yao mwaka 2015 rafiki yao Raila aliwageuka na kumuunga mkono adui ya Rais John Pombe Magufuri

 Mh: Mwenyekiti wa Chadema Taifa Fredrick Mboye

Jumatano, 24 Mei 2017

'Nampenda sana Profesa Muhongo, pia ni rafiki yangu,lakini kwa hili (Makontena ya Mchanga) ameshindwa kuwajibika,namuomba ajitafakari,ajitathimini ninamshauri pia aachie madaraka''
Rais Dk John Pombe Magufuli 24 Mei 2017 Saa 5.18 Asubuhi,Ikulu Dar Es Salaam.
 Rais John Pombe Magufuri

Jumanne, 23 Mei 2017

mcholaji wa nembo ya taifa almahalufu kama bibi na bwana anaishi kwa tabu na kuomba misahada   anaishi  katika hari duni tofauti na mchango wake alio utoa ktk taifa

Vijana wa chama cha mapinduzi (Ccm) ni vijana wanao lelewa katika maadili,Nidhamu na ukakamavu wa hari ya juu vijana hao hupewa fulsa ya kufundishwa juu ya nchi yao hii ni tofauti na mizingi ya vyama pinzani nchini Tanzania.
kutokana na kupewa wasaa wa kuijua vizuri nchi yao basi huwa wajasili na wasio yumbishwa na ushawishi wa vyama pinzani pia vijana hao hubishana kwa hoja na si ubishi usiokuwa na msingi
Vijana wa Ccm

Jumapili, 21 Mei 2017



Bunge la bajeti linaloendelea mjini Dodoma limeghubikwa na mijadala mingi na ya kusisimua ikihusisha hoja nzito zinazotoka kambi za upinzani na CCM, huku pia mawaziri wa kale na wapya wakionekana kana kwamba wana ‘ligi’ yao.

Wakati aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Charles Kitwanga ‘akipambana’ na Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Gerson Lwenge alipochangia kuhusu suala la maji jimboni kwake, Waziri wa zamani wa Habari, Utamaduni na Michezo, Nape Nnauye alionyesha msuli wake katika suala maji jimboni kwake.

Kitwanga alieleza kuwa yale aliyochangia kwenye bajeti ya Wizara ya Maji na Umwagiliaji bungeni ni kama ali-‘beep’ ila mazito yanakuja.
Hata hivyo, Lwenge alimjibu Kitwanga kuwa kama haoni mambo Serikali ilifanya katika wilaya yake ajiondoe katika chama hicho.
“Sasa anaposema anakwenda kuhamasisha wananchi wakabomoe mtambo wa Ihelele maana yake analeta uasi au hathamini kazi iliyofanywa na chama chake,” alisema.
 

Ijumaa, 19 Mei 2017



Kwa muda wa wiki moja sasa kampuni ya Sahara Communications Limited, wamiliki wa Star TV na vyombo vingine vya habari kupitia mitandao ya kijamii wanasambaza taarifa kuwa watafanya mahojiano maalum na Mkuu wa Mkoa wa Dar ea Salaam, Paul Makonda, Jumatatu Mei 22, 2017.

Kusudio hilo la Star TV limekuja wakati kiongozi huyo akiwa amefungiwa na vyombo vya habari kwa uamuzi ulioitikiwa kwa pamoja baina ya Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) na Umoja wa Klabu za Waandishi wa habari Tanzania (UTPC) na kuungwa mkono na Chama cha Wamiliki wa Vyombo vya Habari Nchini (MOAT) na taasisi nyingine za kihabari nchini. Uamuzi wa kumfungia Makonda uliotangazwa Machi 2017, ilitokana na kiongozi huyo kuvamia Kituo cha Utangazaji cha Clouds Madia, March 17, 2017 akiwa na askari wenye bunduki.

Uvamizi wa Clouds ulikuwa mwendelezo wa matukio ya RC Makonda kudhalilisha wanahabari, kutukana na kutoiheshimu taaluma ya habari. Katika tamko hilo, Makonda tulimpa masharti mepesi kurejesha uhusiano na tasnia ya habari, ambayo ni kuomba radhi waandishi wa habari kwa tukio la Clouds na matukio mengine kwa ujumla wake kama sehemu ya uungwana wa Kitanzania.

Tulisema katika tamko kwa yeyote atakayeshirikiana na Makonda naye tutamhesabu kama adui wa tasnia ya habari nchini. Kwa mantiki hiyo tunasema ikiwa Star TV wameamua kushirikiana na Makonda, basi ni wazi wameamua kwa hiyari yao wenye kujitangaza kama adui wa tasnia ya habari nchini.

Kila Mtanzania anajua jinsi ya kupambana na adui kwa namnaya kujilinda, na tasnia haitasita ku fanya hivyo. Kadhalika hivi sasa TEF tunafuatatilia kwa karibu uhusiano wa Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo na vyombo vya habari kutokana na matukio ya mara kwa mara ya kudhalilisha wanahabari wanapokuwa kazini kwa amri yake. Matukio haya yakiendelea, tutalazimika kupitia uhusiano wa RC Gambo na vyombo vya habari nchini.

Mwisho, tunavipongeza vyombo vya habari, kwa maana ya magazeti, radio, televisheni na mitandao ya kijamii ndani na nje ya nchi kwa kutekeleza uamuzi wa kumfungia RC Paul Makonda kwa uaminifu uadilifu wa hali juu, licha ya vishawishi vya hapa na pale vinavyotolewa na wapambe wake.

Nguvu yetu ipo katika umoja wetu kama wanahabari. Tusiipoteze Mungu ibariki Tanzania.

Deodatusi Balile
Makamu Mwenyekiti Jukwaa la Wahariri Tanzania.
Mei 19, 2017
Msichana mwenye umri wa miaka 18, ‘Mangli Munda’ alazimishwa na wazazi wake kufunga ndoa na Mbwa huko nchini India, kufanya hivyo ilikuwa ni imani kufukuza roho za kishetani na mikosi inayomsonga na Mbwa huyo alitafutwa na Baba mzazi wa mrembo huyo na kufanya sherehe kubwa na kufanya vitendo vyote vinavyofanywa na bibi harusi kwa taratibu za ndoa, kwa mujibu wa Yahoo News, msichana huyo hakuwa na furaha kabisa na alieleza wazi jinsi alivyochukizwa na kitendo hicho,“Sifurahii kabisa hii ndoa coz tulilazimika kutumia pesa nyingi kwa ajili ya ya hii ndoa.
Hiyo ndiyo njia pekee tunayofanya kuondoa mikosi kwa kufanya tendo jema kwa ajili ya kijiji chetu.” Amekaririwa mama yake Munda.

Jumatatu, 15 Mei 2017

Jana tar 14/05 kulikuwa na tamasha la vijana ambalo liliandaliwa na mwenyekiti wa mtaa wa kivule Mh.Mzava tamasha hilo la hamasa kwa vijana wafanye kazi lilihudhuliwa na wazanii mbalimbali ambao walitumbuiza katika stage miongon mwao ni G love,mister A,,Buzzuki, na nk nahawa ni wasanii miongoni mwao ni G love na Buzzuki wanatuelezea walivyo kiwasha stageni na nini maon yao katika tamasha hilo

Jumapili, 7 Mei 2017

MMOJA wa wazazi ambao watoto wao wamefariki katika ajali ya gari iliyosababisha vifo vya wanafunzi 33 wa Shule ya Msingi Lucky Vincent, alikuwa miongoni mwa mashuhuda wa ajali hiyo pasipo kujua kama mtoto wake, Justine Alex, alikuwamo katika msafara wa gari hilo.
Mzazi huyo, aliyetambulika kwa jina la Lemburis Saruni, inadaiwa kuwa alishuhudia ajali hiyo akiwa kwenye gari la nyuma, huku lile lililobeba wanafunzi hao likiwa mbele.
ndugu wa karibu na Lemburis ambaye hakutaka jina lake litajwe , alisema baada ya kuona gari hilo limeanguka kwenye korongo alilazimika kushuka ili kwenda kuangalia bila kujua kama mtoto wake ni miongoni mwa waathirika wa ajali.
“Hiyo ajali imeua ndugu zangu, akiwamo mtoto wa baba yangu mdogo, na yeye leo alikuwa anakwenda Ngorongoro, alifuatana na hilo basi la wanafunzi bila kujua na kaliona likidondoka, akashuka akalifuata akakuta mwanawe ndio yupo ananing'inia mlangoni,” alisema ndugu huyo.
Alisema baada ya kumuona akiwa katika hali hiyo, alilazimika kumwondoa na kumuweka pembeni, lakini kwa bahati mbaya alikufa akiwa amemshika mkononi.
Alisema Justine alikuwa mtoto pekee wa Lemburis. Alisema mama wa Justine alifariki dunia mwaka juzi.
Mwandishi wa habari hii alijaribu kumtafuta mzazi huyo kwa njia ya simu ya kiganjani ili aweze kuelezea tukio hilo, lakini hakupatikana hewani.
Mbali na mtoto huyo, mtoa taarifa alibainisha kuwa ajali hiyo huenda ikawa imesababisha vifo vya ndugu zao wengine watano ambao walikuwapo katika msafara huo, ambao ni wanafunzi na walimu.
Chama cha mapinduzi Ccm kimetoa salamu zake za rambilambi kwa ndugu na jamaa wa wanafunzi waliopata ajali huko arusha
Barua toka kwa ccm

Chama tawala nchini Tanzania kinachoitwa Chama cha mapinduzi (CCM) huwa kina kawaida ya kipekee Barani Afrika kwa kutengeneza viongozi watakao kuja kutawala nchini humo na viongozi hao wanaoandaliwa kwa ajili ya kuja kuongoza baadae ni vijana
vijana wa ccm
Vijana hao hukuzwa kwa nidhamu ukakamavu na uwadilifu.. 
Tamaduni hii ya kuandaa vijana kuwa viongozi ni yakipekee kabisa balani Afrika na hata nchini Tanzania mmoja kati ya vijana ambao waliandaliwa vyema kuja kuwa kiongozi wa Tanzania ni Rais mstafu wa Awamu ya 4 Mh.Jakaya mlisho kikwete

Historia Fupi ya Rais mstaafu wa Jamuhuri ya muungano wa Tanzania Mh.Jakaya M. Kikwete


Asili.

Amezaliwa 7 Oktoba 1950 katika kijiji cha Msoga, kata ya Lugobatarafa ya Msoga,jimbo la uchaguzi la ChalinzeWilaya ya Bagamoyomkoa wa Pwani.
Alizaliwa katika familia ya wanasiasaBabu yake Mzee Mrisho Kikwete alikuwa chifuwa Wakwere. Baba yake alikuwa Mkuu wa Wilaya PanganiSame na Tanga.
Jakaya Kikwete amesimulia hadithi ya kifamilia ya kuwa wakati mama yake alipokuwamja mzito naye, babu alitamka kuwa ikiwa mtoto atakuwa wa kiume atampatia urithiwa cheo chake.

Masomo

Miaka 1958 – 1961 akasoma Shule ya Msingi Msoga, halafu 1962 – 1965 Shule ya Kati (Middle School) Lusonga, halafu Shule ya Sekondari Kibaha akiongeza A-level huko Shule ya Sekondari Tanga.
Kuanzia mwaka 1972 alisoma uchumi katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaamakimaliza kwa kupata digrii yake mwaka 1978.
Akajiunga na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).
Jakaya aliposoma Shule ya Sekondari ya Kibaha alikuwa mwenyekiti wa wanafunzina pia wa Vijana wa TANU. Katika Shule ya Sekondari Tanga alikuwa Kiranja Mkuuna pia kiongozi wa timu ya mpira. Katika UDS alichaguliwa kuwa mwenyekiti wahalmashauri ya wanafunzi.

Kupanda ngazi katika siasa

1mwaka huu alikuwa mkulima wa Msoga. Mwaka 1988 akateuliwa kuwa mbunge nawaziri msaidizi. Mwaka 1990 alichaguliwa kuwa mbunge wa Bagamoyo/Chalinzeakirudishwa kila uchaguzi hadi mwaka 2000. Akawa waziri akipita katika wizara zamaji na fedha.
Mwaka 1995 alijaribu kuchaguliwa kuwa mgombea wa urais upande wa CCM. Inasemekana ya kwamba Mwalimu Julius Nyerere alimwomba wakati ule kumwachia nafasi Benjamin Mkapa aliyeteuliwa na Halmashauri Kuu ya CCM. Kikwete akawaWaziri wa Mambo ya Nje katika serikali zote mbili za Mkapa.
Mwaka 2005 alifaulu kuteuliwa mgombea wa CCM kwa nafasi ya rais akashinda uchaguzi wa Desemba 2005 akizoa 80% za kura zote.
Kutokana na Historia Hii fupi Tunaona jinsi Rais mstafu Jakaya mrisho kikwete alivyo andaliwa vizuri kisiasa na kuja kuwa kiongozi mzuri wa Jamuhuri ya muungano wa Tanzania....
Napenda kushauli vyama pinzani au vyama vya kisiasa kufata mfumo huu wa kuandaa viongozi tangu wakiwa wadogo ili kuweza kuja kupata viongozi bora wa baadae

Alhamisi, 27 Aprili 2017

Jina la music anaitwa Mika bwai ila jina lake halisia toka kwa wazazi wake ni Michael Shamba Alianza music akiwa mdogo sana pale kiwalani safari yake ya kimusic ilikuwa ndefu sana.. Alipata nafasi ya kushiliki katika shindano la the jump off michano iliokuwa ikilatibiwa na Times Fm Tz mtangazaji alikuwa Jabil Sarehe a.k.a kuvichaka au kibonge toze shindano hilo lilikwa na washiliki 300 ila kutokana na juhudi binafsi za mika bwai alifanikiwa kufika top 10 ana kuweza kuendelea mbele
mika bwai

Leo msanii huyu anashilik katika shindano la nani mkali wa flow toka ktk blog yetu hii ya Mo dadyTv je ataweza kutusua kama alivyo tusua Times FmTz...

leo tulikuwa na wakali wawili wa hip hop Sir killer na Mo flavour Tz  katika kipengele cha nani mkali wa michano (mkali wa flow) ambao wamepimana nguvu ya rap huu mpambano ulikuwa mkali mno mpaka sasa atuja pata mshindi sasa basi comment nani mshindi bonyeza link => kupata mpambano huo ili uweze kutoa comment yako 
 http://www.mediafire.com/file/7ci486hj6c628ic/Nani_mkali_wa_flow_episod_1._Sir_killer_vs_Mo_flaver.wav

Jumatatu, 10 Aprili 2017

Siku zote kwenye nia kuna njia pia usione vyaelewa vimeundwa leo tutamzungumzia rapper mashuhulu wa Arusha anaefahamika kama Sham shila pia ni hit wa nyimbo mbalimbali kama #nisamehe na nk rapper huyu amejizolea umaalufu mkubwa kutokana na nyimbo zake kali inasemekana alianza kufanya music wa hip hop akiwa mdogo lakin alikuja kuibuka na kufanya show yake wa kwanza nchin uganda show hiyo ilikuwa inaitwa DOADOA MUSIC FESTIVAL 2013 UGANDA. na hii ndio picha yake ktk show hiyo
tuendelee kumsapa ushilikiano wa dhati.......  mchumia juani hulia kivulini

Jumamosi, 1 Aprili 2017

Baada ya hit song ya kisingeli inayoitwa nishuke wapi ya Reall Voice leo amesema anajiandaa kuachia nyimbo nyengine mpyaaaa maneno ya real Voice hivi leo on facebook {Niwakat wakuvut subira mashabik zang kwa new song hatar sanaa yaan Amazing song 2017>> Kwawale walio achwa nawalio acha nawanao pendana kwa dhat hii ni spexh kwenu naamin mtanipend <<love song>>}
Real Voice

Jumanne, 28 Machi 2017

kimbunga kikali kinatarajiwa kupiga pwani ya Australia ya Queensland muda mfupi pamoja na upepo mkali na mvua kubwa
Maelfu ya wakazi wameondolewa kutoka miji ya pwani, na kuacha nyumba zao zikijaa maji.
Gavana wa Queensland, Annastacia Palaszczuk, amesema kwa sasa watu wanapaswa kuchukua tahadhari kubwa na watu hawapaswi kutembea hovyo.
Wafanyakazi elfu mbili wa dharura wanasubiri na kujiandaa kufika katika eneo hilo kutoa msaada kwa kadri itakavyohitajika.
Taarifa za wataalam wa mambo ya hali ya hewa wanasema upepo unatarajiwa kuvuma kwa kilomita 280 kwa saa moja.
Serikali ya Yemen imesema watu 11 waliuawa katika shambulio la kujitoa muhanga kwenye uwanja mmoja Kusini mwa nchi hiyo.

Maofisa wanasema kuwa gari dogo likiwa na vilipuzi, liliendeshwa mpaka kwenye uwanja wa serikali wa al-Houta uliokuwa na mkusanyiko wa watu.
Baadhi ya watu waliokuwa wamevalia mavazi ya kijeshi walitoka kwenye gari hilo na kuanza kushambulia raia na kisha bomu kwenye gari hilo lililipuka.
Shambulizi hili linatajwa kufanywa na kundi la Islamic State ambalo mpaka sasa hawajatoa tamko lolote.

Jumatatu, 27 Machi 2017

rais john pombe magufli ameagiza wimbo mpya wa ney wa mitego_wapo uwachiwe pia aboreshe vitu mbalimbali ktk wimbo huyo

Baraza la Sanaa ka Taifa (BASATA) limeufungia rasmi wimbo ‘WAPO’ uliombwa na msanii wa Bongo Fleva, Nay wa Mitego kutumika kwa namna yoyote ile.
Kwa mujibu wa BASATA kifungu namba 4(L) cha Sheria ya BASATA namba 23 ya mwaka 1984, Baraza limepewa jukumu la kusimami kazi za Sanaa na mamlaka za kishirika kuhakikisha yote yafanyikayo katika tasnia ya Sanaa hayaachi taifa na wasanii katika hali sizizo salama.
Katika kutekeleza majukumu haya, Baraza linahakikisha linalinda maadili miongoni mwa wasanii wanapokuwa jukwaani au wanapobuni kazi zozote za sanaa.
Kwa muda huu, BASATA linawakumbusha wasanii na wadau wote wa kazi za sanaa kuzingatia ubunifu wa hali ya juu kufanya kazi za Sanaa, hata kufikisha jumbe mbalimbali za kufundisha, kuelemisha, kuburudisha hata kuonya.
Baraza linawaonya wale wote wanatumia kazi zilizopigwa marufuku, ikumbukwe kuwa kutumia kazi zilizopigwa marufuku ni ukiukwaji wa sheria za nchi,  hatua kali zitachukuliwa juu yao.
Maelfu ya raia wamekusanyika katika maeneo tofauti nchini Urusi wakiandamana kupinga kile wanachodai matumizi mabaya ya fedha za umma.

Mkusanyiko mkubwa upo katika mji wa Moscow ambapo shinikizo ni kumtaka waziri mkuu wa Urusi Dmitry Medvedev kujiuzulu.
Wanaharakati wanasema kuwa hadi sasa watu 800 wanashikiliwa na Polisi.
Maandamano haya yanatajwa kuwa ni makubwa zaidi ya yale yaliyowahi kutokea nchini Urusi kwa miaka mingi, ambapo wanadai kuwa waziri mkuu wao Dmitry Medvedev amekuwa akutumia fedha za umma
katika mambo yake binafsi kwa kujenga majumba kifahari, kununua boti za kifahari, mashamba ya mvinyo na jumba la kufugia bata.
Katika viunga vya Pushkin mjini Moscow, kuna kundi kubwa la waandamanaji waliokusanyika, mmoja wao amesema kuwa fedha za serikali zinaibiwa.
Marekani imeilaumu Urusi kwa hatua yake ya kuwashikilia mamia ya waandamaji kwa madai kuwa wanavuja haki dhidi ya maandamano ya amani kwa mujibu wa haki za binadamu.