mo dadyTV

KARIBU KUTANGAZA NASI 0652231836

kARIBU KUTANGAZA NASI 0652231836

LightBlog
KARIBU KUTANGAZA NASI 0652231836

Karibu kutangaza nasi mawasiliano 0652231836

Jumatatu, 28 Novemba 2016

November 29, 2016 U Heard ya Soudy Brown ndani ya XXL ya Clouds FM iko na story kuhusu uhusiano wa kimapenzi uliokuwepo kati ya rapa Young Dee ambaye aliwahi kuwa na uhusiano na Video Queen Tunda waliyeacha baada ya kutoelewana kupelekana polisi.
Baada ya kuwepo taarifa kwamba Tunda ameachwa na mwanaume anayetajwa kuwa alikuwa akimgharamia kwa kila kitu ikiwemo kulipia nyumba, kununua magari na starehe zote alizokuwa akizifanya kila siku, ikaja kuonekana ameanza kuwa karibu tena na Yo
Leo Soudy Brown amepiga stroy na Young Dee ambaye ameeleza kuwa yeye na Tunda wako vilevile kama mwanzo hawakuwahi kugombana na ameamua kumsamehe Tunda kwasababu itakuwa kosa kubwa endapo hatamsaheme wakati yeye pia ana makosa makubwa zaidi ya hayo ya Tunda.
ung Dee.
“Mimi nilikuwa na matatizo yangu mengi sana hata kufika hapa tu nimesamehewa sana vitu vingi katika watu ambao hawakutakiwa kusamehewa ni mimi ndio mana nimeamua kumsamehe, kwa yote ambayo Mungu amenisamehe nisiposamehe nitakua nakosea sana” – Young Dee
Jeshi la Polisi Dodoma linawashikilia watu tisa kwa tuhuma za uhalifu wa kuvunja nyumba na kuiba mali za watu, kaimu kamishna wa jeshi la polisi kanda ya Dodoma Kimora Ernest amesema wahalifu wote wamekamatwa ndani ya siku mbili mfululizo huku likiwataka wananchi waliowahi kuibiwa mali zao kujitokeza kubaini kama zipo kati ya zilizokamatwa.

Jeshi la polisi Dodoma tunawashikilia watu tisa kwa tuhuma mbalimbali zikiwamo za wizi, katika msako wa siku mbili tuliweza kufanya msako huo ambapo wanawake ni watatu na wanaume sita‘ –Kimora Ernest
Mtandao wa wahalifu hao ni mkubwa ukilinganisha na mitandao mingine kutoka mikoa mbalimbali, zoezi la msako linaendelea ili kumaliza msako huu‘ –Kimora Ernest
Mbinu wanazotumia wahalifu hawa ni kuvunja nyumba hasa nyakati za usiku na mchana pale wanapobaini kuwa wenyeji hawapo katika nyumba zao. Nitoe wito kwa wananchi kujiepusha na tabia ya kununua vitu mitaani visivyokuwa na risiti pia tuwatake wale wote waliowahi kuibiwa katika kipindi kama hiki wajitokeze kubaini kama kati ya mali zilizokamatwa ni zakwao‘ –Kimora Ernest
Victoria Secrete 2016 supermodels akiwemo Mtanzania Herieth Paul, Kendall Jenner etc wametua jijini Paris tayari kwa ajili ya show hiyo kubwa ktk Fashion World itakayofanyika tarehe 5 December.

Models wa kibongo ambao wengine mmeridhika Kuwa wahudumu ktk events just be inspired

Ijumaa, 18 Novemba 2016

Kiungo wa kimataifa wa Ujerumani anayecheza Man United ya England Bastian Schweinsteiger ameshinda tuzo ya heshima ‘Special Jury’ kwa mchango wake katika timu ya taifa ya Ujerumani, Bastian ameshinda tuzo hiyo licha ya kuwa katika kipindi kigumu chini ya Mourinho.

Bastian ambaye ametangazwa mshindi wa tuzo hiyo inayoandaliwa na vyombo vya habari vya Ujerumani na kujulikana kwa jina kama la Bambi Awards, ametangazwa kuwa mshindi wa tuzo hiyo kwa ushirikiano wake, pamoja na kocha wao wa timu ya taifa ya Ujerumani Joachim Low ameshinda tuzo kwa ushirikiano wake timu ya taifa.

                                                 Bastian na mkewe Ana Ivanovic

Kiungo huyo ambaye aliambatana na mkewe ambaye ni mchezaji tennis Ana Ivanovic, alitangaza kustaafu kucheza timu ya taifa ya Ujerumani mwezi August 2016, Bastian amefanikiwa kushinda kombe la dunia akiwa na timu ya taifa ya Ujerumani mwaka 2014.
Rais wa shirikisho la soka ulimwengu FIFA Gianni Infantino anapanga kuboresha michuano ya klabu Bingwa dunia kutoka timu 7 hadi timu 32 lengo likiwa ni kuboresha michuano hiyo ili ilete mvuto tofauti na ilivyokuwa sasa.

Gianni Infantino ametoa wazo hilo na kutazamiwa lianze kufanyiwa kazi katika michuano ya klabu Bingwa dunia kuanzia mwaka 2019, michuano hiyo kwa sasa inashirikisha timu 7 kitu ambacho kinatajwa kutokuwa na mvuto na kufanya mshindi iwe rahisi kumtabiri.

Rais huyo anaamini kubadili mfumo huo kutafanya kuongeza mvuto wa mashindano hayo, ambapo karibia kila mara Bingwa wa Ulaya na America Kusini ndio huwa wanakutana fainali, Infantino anaamini mashindano hayo yakiwa yanachezwa kuanzia June 10 hadi June 30 yakishirikisha timu 32 yatakuwa na mvuto.
Kiungo wa kimataifa wa Ubelgiji anayeichezea Chelsea ya London Eden Hazard November 18 2016 alitangazwa mshindi wa tuzo ya mchezaji bora wa mwezi October, baada ya kucheza mechi nne, kufunga goli tatu na kutoa assist katika ushindi wa Chelsea wa mechi zote nne.
Eden Hazard ambaye amekuwa akitajwa kuhitajika kwa miaka kadhaa sasa na klabu ya Paris Saint Germain (PSG) ya Ufaransa na kuwa amekuwa akisisitiza kuwa na furaha katika klabu ya Chelsea, ameweka wazi kuwa anaweza kuondoka Chelsea ila ni baada ya kutwaa Ubingwa.

“Ndio naweza kuondoka Chelsea siku moja lakini ni baada ya kuisaidia kutwaa Ubingwa, unahitaji kucheza vizuri na kwa kujitoa ili watu waweze kukukumbuka kwa sababu za msingi”

Jumapili, 13 Novemba 2016

1. kunasiku nilichelewa kufika skull ile kufika tu nikamkuta ticha yupo class alivyo niuliza kwanini nimechelewa sindo nikamjibu nguo zangu za shule jana usiku nilivyo fua ziliibiwa alafu mwizi leo kachelewa kuludisha daah! acha nichezee mikwaju kwakumdanganya tisha
2. kuna mdem huyo nilikuwa na mahusiano nae siunajua kikati ya mapenzi tena akabidi abadilishe jina la nikki name akaanza na jina lake mwisho dady likatamba kila mtu akawa analijua sindo tukagombana bhana akipita mtaani akiitwa jina lake tu lile la nikki name mitusi hatali hasa nani alimtuma ajipe sindo washkaji wakanambia kuwa na hule demu nimepuyanga maana sio taipu yan
gu
Shirika la utangazaji Uingereza BBC November 12 2016 limetangaza majina ya wachezaji watano wa Afrika wanaowania tuzo ya mchezaji bora wa mwaka 2016 wa BBC, majina hayo matano yametajwa live katika kipindi cha TV.

Tuzo hiyo ya BBC 2016 mshindi atatangazwa December 12 2016 live kupitia  BBC Focus On Africa TV na radio,list ya majina matano yaliochaguliwa.

  • Sadio Mane (Liverpool/Senegal)
  • Yaya Toure (Man City/Ivory Coast)
  • Riyad Mahrez (Leicester City/Algeria)
  • Andrew Ayew (West Ham United/Ghana)
  • Pierre-Emerick Aubameyang (Borussia Dortmund/Gabon)
Wanawatangazia nafasi za usanii kwa wale wenye vipaji,fani na taaruma kama ni mmoja wapo kati ya hivi njoo chimpo arts group utimize ndoto zako...
tunashuhulika na sanaa za MAIGIZO,NGOMA,MUSIC,MITINDO,UPAMBAJI MAKEUP,MATANGAZO Na NK

tunapatikana Temeke buza kanisani ukumbi Ngara pub
kwa mawasiliano zaidi unaweza ukapiga simu: 0657574884/0689318881/0652231836

kaulimbiu yetu: CHIMPO: {sanaa na taaluma fani na vipaji}