mo dadyTV

KARIBU KUTANGAZA NASI 0652231836

kARIBU KUTANGAZA NASI 0652231836

LightBlog
KARIBU KUTANGAZA NASI 0652231836

Karibu kutangaza nasi mawasiliano 0652231836

Jumamosi, 4 Machi 2017

Trump asema Obama alikuwa akidukua simu yake

Rais wa Marekani Donald Trump amemshutumu mtangulizi wake kwa kudukua simu yake mwezi mmoja kabla ya kuchaguliwa kuliongoza taifa hilo.
Rais Trump alichapisha ujumbe wa Twitter mapema siku ya Jumamosi akisema: Makosa sana! Nimegundua kwamba rais Obama alikuwa akidukua simu yangu katika afisi yangu iliopo Trump Tower kabla ya mimi kupata ushindi .


Aliongezea kwamba awali mahakama moja ilipinga uchunguzi kuhusu kudukuliwa kwa simu yake.
Rais huyo wa Marekani hajatoa ushahidi wowote ili kuthibitisha madai hayo ama hata kusema ni agizo gani la mahakama alilonukuu.
Ripoti za vyombo vya habari zimesema kuwa shirika la kijasusi la FBI liliomba agizo la kuwachunguza maafisa wa karibu wa Rais Trump kutoka kwa shirika la kigeni la kijasusi Fisa kubaini iwapo wamekuwa wakiwasiliana na maafisa wa Urusi.
Agizo hilo lilikataliwa lakini baadaye likakubaliwa mwezo Oktoba kulingana na ripoti hizo za vyombo vya habari.
Hakujakuwa na thibtisho rasmi na pia haijulikani iwapo hatua hiyo ilichunguzwa.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni