mo dadyTV

KARIBU KUTANGAZA NASI 0652231836

kARIBU KUTANGAZA NASI 0652231836

LightBlog
KARIBU KUTANGAZA NASI 0652231836

Karibu kutangaza nasi mawasiliano 0652231836

Jumapili, 5 Machi 2017

Mexico yafungua vituo miji 50 nchini Marekani kutetea raia wake



Mexico imefungua vituo vya kutoa msaada wa kisheria katika balozi zake katika miji 50 ya Marekani, ili kulinda raia wake kutokana na utekelezaji mkali wa sheria za uhamiaji nchini humo.

    Wakati wa ziara ya maafisa wakuu wa Marekani nchini Mexico mwezi uliyopita, utawala wa nchi hiyo ulielezea wasiwasi wake juu ya sera ya Trump ya uhamiaji dhidi ya raia wake.

    Vituo hivyo vipya vitatoa msaada wa sheriak wa raia wa Mexico ambao wanahisi kuwa haki zao ziko hatarini nchini Marekani.
    Uhusiano kati ya Mexico na Marekani umekuwa mbaya zaidi tangu miango kadha iliyopita.
    Wiki moja baada ya kuapishwa mwezi Januari , Rais Donald Trump alisema kuwa atajenga ukuta kati ya mpaka wa Mexico na Marekani.
    Alisisitiza kuwa Mexico italipia gharama ya ujenzi wa ukuta huo.
    Matamshi hayo yalisababisha rais wa Mexico Enrique Pena Nieto, kufuta safari yake nchini Marekania tarehe 31 mwezi Januari. na kutangaza ufadhili zaidi kulinda haki za za raia wa Mexico walio nchini Marekani.

    Hakuna maoni:

    Chapisha Maoni