Jeshi la
Polisi Dodoma linawashikilia watu tisa kwa tuhuma za uhalifu wa kuvunja
nyumba na kuiba mali za watu, kaimu kamishna wa jeshi la polisi kanda ya
Dodoma Kimora Ernest
amesema wahalifu wote wamekamatwa ndani ya siku mbili mfululizo huku
likiwataka wananchi waliowahi kuibiwa mali zao kujitokeza kubaini kama
zipo kati ya zilizokamatwa.
‘Jeshi
la polisi Dodoma tunawashikilia watu tisa kwa tuhuma mbalimbali
zikiwamo za wizi, katika msako wa siku mbili tuliweza kufanya msako huo
ambapo wanawake ni watatu na wanaume sita‘ –Kimora Ernest
‘Mtandao
wa wahalifu hao ni mkubwa ukilinganisha na mitandao mingine kutoka
mikoa mbalimbali, zoezi la msako linaendelea ili kumaliza msako huu‘ –Kimora Ernest
‘Mbinu
wanazotumia wahalifu hawa ni kuvunja nyumba hasa nyakati za usiku na
mchana pale wanapobaini kuwa wenyeji hawapo katika nyumba zao. Nitoe
wito kwa wananchi kujiepusha na tabia ya kununua vitu mitaani
visivyokuwa na risiti pia tuwatake wale wote waliowahi kuibiwa katika
kipindi kama hiki wajitokeze kubaini kama kati ya mali zilizokamatwa ni
zakwao‘ –Kimora Ernest
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni