mo dadyTV

KARIBU KUTANGAZA NASI 0652231836

kARIBU KUTANGAZA NASI 0652231836

LightBlog
KARIBU KUTANGAZA NASI 0652231836

Karibu kutangaza nasi mawasiliano 0652231836

Ijumaa, 18 Novemba 2016

Mipango mipya ya Rais wa FIFA kuhusu klabu Bingwa dunia kuanzia 2019

Rais wa shirikisho la soka ulimwengu FIFA Gianni Infantino anapanga kuboresha michuano ya klabu Bingwa dunia kutoka timu 7 hadi timu 32 lengo likiwa ni kuboresha michuano hiyo ili ilete mvuto tofauti na ilivyokuwa sasa.

Gianni Infantino ametoa wazo hilo na kutazamiwa lianze kufanyiwa kazi katika michuano ya klabu Bingwa dunia kuanzia mwaka 2019, michuano hiyo kwa sasa inashirikisha timu 7 kitu ambacho kinatajwa kutokuwa na mvuto na kufanya mshindi iwe rahisi kumtabiri.

Rais huyo anaamini kubadili mfumo huo kutafanya kuongeza mvuto wa mashindano hayo, ambapo karibia kila mara Bingwa wa Ulaya na America Kusini ndio huwa wanakutana fainali, Infantino anaamini mashindano hayo yakiwa yanachezwa kuanzia June 10 hadi June 30 yakishirikisha timu 32 yatakuwa na mvuto.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni